DRC
DRC Wakimbizi wa Vita mashariki mwa Congo waomba kurejea nyumbani kutokana na mateso wanao pitia katika kambi mbali mbali .
Wakishudia mvua kali kwa sasa katika hema zao ambako waishi katika kambi mbali ,wakimbizi wa vita mashariki mwa Congo waomba kurejeshwa kwenye vijiji vyao kwani wamechoka na Maisha ya kuishi katika hema .
Mmmoja wa wkaimbizi alie hifadhi jina lake asema ,kwa sasa amejikuta na maradhi ya msongo wa mawazo kutokana na Maisha anayo ishi kwa sasa akiwa na Watoto kambini bila kusoma .
Mama huyu anasema kila siku anaondoka asubui kambini kutafuta kuni katika mbuga la Wanyama pori la Virunga pembeni ya kambi yake ya Bulengo lakini hukutana na watu wenye silaha wanao baka wanawake.