DRC-Goma

MAONI YA WAKAAJI WA MUJI WA GOMA KUHUSU SHEREHE ZA KUAPISHWA KWA RAISI WA DRC...

JANUARI 19, 2024
Border
news image

Prince Makuke wa umuri ya miaka thelatini na nane akiwa baba wa watoto tatu mukaaji wa muji wa Goma, anena kwamba yeye asubiri kwa hamu kubwa kuapishwa rasmi kwa Rais wa DRC Felix Antoine Tshisekedi Tshilombo hii juma mosi tarehe ishirini January elfu mbili ishirini na ine mjini Kinshasa. Sherehe hizo zitafanyika kwenye uwanja WA kandanda wa mashahidi(des matures ) .

Alinena ya kwamba ana subiri kwa hamu sana sherehe hiyo ambayo ita mupelekeya rais wa DRC kuanja rasmi kazi ya muhula wake wa miaka tano ijayo. Mwana inchi huyu aomba kwa rais wa DRC kuchukua ma jukumu yake yote kwa ajili ya kudumisha usalama na inchini DRC hususani jimboni kivu ya kaskazini ambayo imekumbwa na matatizo kwa muda miaka mingi. Mukaaji huyu awaomba piya wale wanao endeleya kupinga matokeo ya ku chaguliwa kwake Felix Antoine Tshisekedi Tshilombo ku raisi kukubali kwani wana inchi wame muchagua na korti kuu ya mahakama ime tibitisha matokeo iliyo tangazwa na tume huru ya uchaguzi inchini Drc CENI akiomba kwa wote kumuunga mukono na kuachana na vurugu inchini.

NDIWELUVULA BIN MUTUME MTV NEWS ONLINE