DRC BUKAVU KIVU KUSINI

Kufungwa kwa Mupaka wa Rwanda na Burundi wa wa Watiya Matatizoni Wenye Shirika za Usafirishaji Mjini Bukavu Wanao Tumiya Njia ya Rwanda.

JANUARI 16, 2024
Border
news image

Wakati uhusiyano wa mataifa jirani Rwanda na Burundi unaendeleya kuwa katika hali ya Utofauti, hali hiyo ya asiri piya uchumi pamoja na muzunguko wa wana inchi wa mataifa mengine yanayo pakana na inchi hizo.

Mutafahamu ya kwamba, tangu siku ya alahamisi ya tariki kumi na moja iliyo pita, wakati serekali ya Burundi ili amua kufunga mipaka yake na Rwanda wenye kuwa na shirika za usafirishaji mjini Bukavu za kwenda Bujumbura kupitiya njia ya Rwanda kwa sasa wana kuwa katika matatizo ya Kusafiri wakitumiya muda murefu kwa kufanya muzunguko kupitiya njia ya bonde la muto Ruzizi huko kamanyola. Na kwa njiya ambayo walikuwa wakitumiya saha ine njiani kupita Rwanda kwa sasa wanatumiya muda wa saha tisa hadi saha kumi kufwatana na uharibifu wa barabara ya taifa nambari tano ya kutoka Bukavu kuelekeya Uvira na kuvuka Bujumbura na kuwa hatarini kwa majambazi wanao jitukiza kila mara kunako njia hiyo na abiriya wa safiri wakiwa na wasiwasi.

NDIWELUVULA BIN MUTUMEĀ  - MTV ONLINE