TANZANIA

BMH YAFANYA MATIBABU YA MOYO KWA KUTUMIA MSHIPA WA MKONO KWA MARA YA KWANZA

FEBRUARI 15, 2024
Border
news image

Hospitali ya Benjamin Mkapa(BMH)nchini Tanzania imefanya uchunguzi wa moyo kwa mgonjwa kwa kutumia mshipa wa mkono kwa mara ya kwanza.

Kwa mujibu wa Mkuu wa kitengo cha maabara maalum ya uchunguzi wa Moyo(Catheterization Laboratory -CathLab) cha Hospitali hio, Dkt Kelvin Masava, uchunguzi na matibabu kwa njia hio mbali na kuwa na faida nyinginezo lakini inampunguzia mgonjwa muda wa kukaa hospitalini.

"Mgonjwa anarejea kwenye shughuli zake kwa wepesi na haraka ikilinganishwa na njia ya kupitia kwenye mshipa wa mguuni tuliyokuwa tukitumia wakiitumiaa awali," anasema.

Anafafanua kuwa utaratibu huu unamuwezesha mgonjwa kunyanyuka na kutembea mwenyewe mara tu baada ya kupata huduma tofauti na apo awali.

"Njia ya mshipa wa mguuni ilihitaji mgonjwa kukaa si chini ya saa sita baada ya huduma pasipo kuinuka kitandani au kukunja mguu tofauti na hii ambapo anainuka kutembea mwenyewe na baada ya saa chache anaweza kuruhusiwa kwenda nyumbani siku hiyo hiyo," ameongeza.

MTV Tanzania