Alhamisi hii, Julai 27, wanafamilia walioathiriwa na vita kati ya jeshi la Congo FARDC na waasi wa M23 waliandaa misa ya mahitaji na maombolezo ya pamoja kuwakumbuka watu Zaidi ya miambili waliouawa katika vita hivyo. Wakongo kadhaa walishiriki misa hii wengi wao kutoka Rutshuru,Masisi na nyiragongo.
Wakaazi hao wameomba mataiafa yaenye nguvu hasa Umoja wa mataifa kuwekea vikwazo wote wanao saidia waaasi wa M23 kwa mbali na karibu ,wakishutumu Taifa Jirani la Rwanda kuwa musatari wa mbele na jeshi lake kusaidia Uasi wa M23 ,M23 Ikiomba mazungumuzo na serikali ya Kinshasa kama njia moja ya kumaliza vita mashariki mwa Congo.
Uasi wa M23 kwa sasa unadhibiti eneo la Rutshuru ,masisi,Nyiragongo ambako kuna wanajeshi kutoka Africa mashariki hasa wanajeshi kutoka kenya,Burundi na Uganda.