DRC

Waziri mkuu wa jamhuri ya kidemikrasia ya Congo Judith Suminwa aonya mawaziri kufanya kazi kwa maslahi ya wananchi

JULAI 24, 2024
Border
news image

Alisema hayo wakati wa kuhitimishwa kwa semina ya uongozi bora kwa mawaziri wapya walio teuliwa na Felix Tshisekedi aiku zilizo pita.

Waziri Mkuu Judith Suminwa alifunga Jumanne hii kikao cha siku mbili ambacho kilishirikisha mawaziri wote wa pya katika ukumbi wa Bunge wa Palais de la Nation, Semina ya Serikali iliyofunguliwa Jumapili iliyopita.

Semina , iliyoandaliwa chini ya kaulimbiu "kuweka makubaliano ya ushiriki wa raia kwa kukuza utendaji kazi katika utawala na utekelezaji mzuri wa mabadiliko katika utekelezaji wa PAG 2024-2028", yenye lengo la kuunganisha umoja wa Utendaji wa kitaifa.

Kwa Rais Tshisekedi, mkataba wa kujitolea kwa raia uliotiwa muhuri ni kutekeleza sera zinazoboresha maisha ya kila Mkongo, bila ubaguzi. "Hili ndilo agizo Muhimu kwa wafanya kazi

"Kwa pamoja, tualikwa kuashiria vyema historia ya nchi yetu kwa kuharakisha mabadiliko yake na kuibuka kwake, kwa kuhakikisha ustawi wa wenzetu," aliendelea Mkuu wa Nchi katika hotuba yake iliyosomwa na Waziri Mkuu.

“Tuna fursa ya kuuonyesha ulimwengu umuhimu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kuwa nchi suluhu. Zaidi ya hapo awali, tupe maana wimbo wetu wa taifa, (Debout Congolais)! ", aliongeza.

Semina ya uongozi bora kwa mawaziri

Mwishoni mwa mikutano hii, pendekezo kadhaa zilitolewa. alibainisha Katibu Mkuu wa serikali Jean Albert Ekumbaki.

AM/MTV News DRC